Jumanne, 27 Februari 2018

CONGO DRC

HABARI Mahakama ya kijeshi kaskazini magharibi mwa DRC imemuhukumu kifungo cha maisha jela afisa wa polisi aliyefyatua risasi na kumuua mmoja wa wandamanaji wanaompinga rais Joseph Kabila. Mjini Kinshasa pia afisa mwingine wa polisi amekamatwa kwa makosa kama hayo na anatarajiwa kufikishwa mahakamani. Hata hivyo, mashirika ya kutetea haki za binadamu yamezungumzia kutoridhishwa na kesi hiyo kwa sababu haiwahusishi viongozi wa ngazi ya juu ambao wanaongoza jeshi na polisi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni