Jumatano, 7 Machi 2018

TAARIFA KUTOKA TFDA

Mamlaka ya chakula na dawa nchini TFDA imesema Tanzania itajiunga na mataifa mengine kuzuia uingizaji wa Soseji kutoka Afrika Kusini zilizobainika kuwa na bakteria aina ya Listeria, iliyosababisha vifo vya watu takriban 180 nchini Afrika Kusini tangu 2017. Tayari Kenya, Zambia, Malawi, Botswana, Zimbabwe, Swaziland na Msumbiji zimepiga marufuku bidhaa za nyama ya kusindika kuingia nchini mwao. Bakteria ya Listeria inasemekana kusababisha homa kali, kuharisha na pia kuwa na athari katika mfumo wa damu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni