Jumatatu, 12 Machi 2018

PIERRE NKURUNZIZA APEWA CHEO NA CHAMA TAWALA

Chama tawala nchini Burundi kimempa cheo cha ''mlinzi aliyetukuka'' rais Pierre Nkurunziza wakati ambapo wakosoaji wake wanadai kwamba anataka kubakia madarakani milele. Katibu Mkuu wa chama tawala cha CNDD-FDD Evariste Ndayishimiye amesema kupitia njia ya vidio katika mkanda uliotumwa kwa shirika la habari la AFP na kuthibitishwa na afisa mmoja, kwamba rais Nkurunziza ni mzee wao,baba yao na mshauri wao. Wakosoaji wamelalamikia kilichotokea wakisema kwamba ni kumpa umaarufu wa kuonekana kuwa ni Mfalme Nkurunziza. Kwa sasa kura ya maoni kuhusu Katiba iliyopangwa kufanyika mwezi Mei mwaka huu huenda ikampa nafasi ya kugombea tena katika uchaguzi wa mwaka 2020 na kumfungulia njia ya kubakia madarakani hadi mwaka 2034.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni